Sunday, July 20, 2014

Tupia Kitenge Ndani Ya Kitambaa Cha Suti Hivii...




HE is The Mighty GOD.

Wazo hili lilinijia ghafla wakati nashona vitambaa vya suti siku za nyuma,kwamba,naweza kutupia ladha ya kitenge kidogo kwenye kitambaa cha suti na kikapendeza.Sasa kwa kuwa mimi napenda makoti,nikaona nitengeneze koti nitupie halafu tuone inakuajekuaje.Nikajiuliza nalitupia kivipi maana sikutaka koti lijae sana kitenge.Nikapata wazo ya koti ambalo nataka nitupie kitenge mahali fulani fulani,nikaprint picha yangu,nikai-modify navyotaka mimi.

Nilitaka sehemu ya chini tu ya koti kutoka kwenye hiyo picha hapo.Nikaanza kuchora vipimo kama kawaida..


Nilitaka liwe na nakshi za vifungo vya kitenge mikononi,mbele na nyuma.Hivyo nikatengeneza vifungo vyangu vitano kama vinavyoonekana pichani

 Nikaona si haba nishone na sketi ya nguva kabisa aka 'mermaid skirt' na nikanogesha na kwenye pochi pia,tayari mie huyoo nimemaliza.
































My natural hair....free-style.Nimekuwa nikipata maswali kuhusu utunzaji wa nywele asilia mara kwa mara.Nitakuja kuzungumzia na hili pia.Kwa kifupi,utunzaji wa nywele asilia ni rahisi zaidi na salama kabisa ukilinganisha na matunzo ya nywele bandia au zenye dawa.Hii mada nitakuja kuiongelea muda si mrefu.

Endelea kutembelea humu kama kawaida.Umependa mishono?whatsup yangu hiyo hapo kulia.
Mpaka wakati ujao,stay classy.Bye.

No comments:

Post a Comment