Saturday, July 26, 2014

JumpSuit With Ankara Flavor By Margareth Tarimo




HE is The Faithful GOD.

Yani kupiga picha hizi ilikuwa ni full burudani.Maana mpiga picha alikuwa hana mbavu kila nikipozi,halafu kulikuwa na kaupepo basi yani anacheka karibu akauke jinsi hili surupwete linavyotepweta.Mimi mwenyewe nilikuwa hoi kwa kucheka.It was so much fun!

Niliwaahidi kuwa nitashona 'kanya humohumo' au jumpsuit hivi karibuni.Ahadi ni deni.Kama kawaida nimetupia na kitenge.Kitenge kwangu ni kama chumvi kwenye chakula.lol!..Haya sasa,hilo hapo muhangaike nalo wenyewe.













 Mbavu zangu!..uwii...naiogopa fashion sasa.







 Kiruu!nauliza tena..umeshawahi kuona mtoto wa kama mwaka mmoja na nusu aliyeachia mizigo yake kwenye pampers jinsi suruali yake inavyomshuka??...






Fashion.It's all about generating good ideas every moment.Some may be funny though.Ila nimejitahidi kuliremba  lipo poa sana halafu lipo soo comfortable.Yani sana.Litanisitiri nikiwa napeleka wanangu shule na kwenda shopping za hapa na pale.Kama unadhani langu ni kituko,angalia hili fungakazi sasa...


                             Asante sana.

Yeah,wakati mwingine fashion ni vichekesho.Tuvae tuchekeshe wengine,wanenepe,waongeze maisha.

Mie kama umelipenda nakushonea tena kali kweli kweli!Tutafutane whatsup +255 712 484508.
Mpaka wakati ujao,stay classy....Bye.

No comments:

Post a Comment